• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Mail za Ofisi |
    • Malalamiko |
TARIME DISTRICT COUNCIL
TARIME DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Mali Asili
    • Kitengo
      • Teknolojia ya Habari na Uhusiano
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Shughuli za Kilimo
    • Shughuli za Ufugaji
    • Shughuli za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Mipango & Utawala
      • Elimu, Afya & Maji
      • Mazingira, Ujenzi & Uchumi
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopangwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Taratibu Mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za Shughuli Mbalimbali
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Ardhi na Mali Asili

IDARA YA ARDHI NA MALIASILI

Idara ya Ardhi na Maliasili ni miongoni mwa Idara kubwa zilizopo katika Halmashauri ya Tarime. Idara hii imegawanyika katika vitengo vikubwa viwili (2) ambavyo ni Kitengo cha Ardhi na Kitengo cha Maliasili.

 KITENGO CHA ARDHI:

Kitengo hiki kinahusika hasa na masuala yote yahusuyo ardhi kwa ujumla ikiwa ni pamoja na Usimamizi wa ardhi, Umilikishaji na udhibiti wa matumizi ya ardhi, Upangaji wa Miji na Vijiji, Upimaji wa ardhi na uthamini. Ni sehemu inayolinda haki, wajibu na maslahi katika ardhi kwa kusimamia sheria, sera na kanuni zinazolinda maslahi katika ardhi. Kitengo hiki pia kinaundwa na vitengo vidogo vinne (4) ambavyo ni Kitengo kidogo cha Mipango Miji, Usimamizi wa Ardhi, Uthamini pamoja na Upimaji na Ramani.

  • KITENGO CHA MALIASILI

Kitengo hiki kimegawanyika katika vitengo vidogo viwili (2) ambavyo ni Kitengo kidogo cha Misitu na Wanyamapori ambazo zinahusika na usimamizi na utunzaji wa maliasili zilizopo katika halmashauri ya Wilaya ya Tarime. Ni kitengo kinachowajibika katika usimamizi wa rasilimali za misitu na Wanyamapori katika halmashauri yetu yenye changamoto nyingi za uvamizi wa tembo na ujangili hasa katika vijiji vinavyopakana na hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Kupitia kada ya Wanyamapori idara ina jukumu pia la kufanya doria na kudhibiti nyara za serikali, kusimamia na kutekeleza sheria Na. 5 ya Wanyama pori ya Mwaka 2009 pamoja na kusimamia shughuli za utalii.

  •  
  • HALI YA WATUMISHI
  • Idara ina jumla ya watumishi ishirini na tatu (23) ambao wamegawanyika katika makundi mawili kulingana na kada zao za kazi na pia vituo vyao vya kazi. Watumishi kumi na sita(16) wapo makao makuu ya wilaya na wengine saba (7) wapo nje ya makao makuu ya wilaya.
  • Jedwali hapo chini linaonyesha idadi ya watumishi kwa kila kada.

Na

KADA ZA IDARA YA ARDHI NA MALIASILI

IDADI YA WATUMISHI

1

UTHAMINI

3

2

USIMAMIZI WA ARDHI

3

3

UPIMAJI NA RAMANI

5

4

MIPANGO MIJI

2

5

MISITU

3

6

WANYAMAPORI

7

JUMLA

23


SHUGHULI MBALIMBALI ZINAZOTEKELEZWA NA IDARA YA ARDHI NA MALIASILI.

 KITENGO KIDOGO CHA MIPANGO MIJI.

Majukumu ya kazi za kila siku za kitengo kidogo cha mipango miji:-

  • Kuandaa michoro ya mipango miji ya matumizi bora ya ardhi katika miji midogo na vituo vya kibiashara.
  • Kuratibu uandaaji wa mipango ya matumizi bora ya ardhi katika vijiji.
  • Kudhibiti ujenzi holela katika miji na vijiji kwa mujibu wa sheria ya mipango miji ya mwaka 2007.
  • Kushughulikia mabadiliko ya matumizi ya ardhi ya viwanja na mashamba.
  • Kuandaa orodha ya maeneo yanayotakiwa kupandishwa hadhi ya kuwa miji midogo.
  • Kushughulikia migogoro mbalimbali ya ardhi.
  • Kuwasilisha michoro ya mipango miji na ramani za matumizi bora ya ardhi ya vijiji Wizara ya Ardhi kwa uidhinisho.
  • Kuishauri kamati ya mipango katika masuala ya kitaalam ya mipango miji.

KITENGO KIDOGO CHA UTHAMINI.

Majukumu ya kazi za kila siku za Kitengo kidogo cha Uthamini:-

  • Kutoa elimu na ushauri wa kitaalam kwa wananchi/Taasisi mbalimbali juu ya masuala ya uthamini wa aina mbalimbali kadiri wanavyohitaji.
  • Kufanya uthamini kwa wananchi/Taasisi mbalimbali kulingana na maombi yanayotufikia.
  • Na mengineyo yanayopangwa na mkuu wa idara/Mkurugenzi Mtendaji.

KITENGO KIDOGO CHA USIMAMIZI WA ARDHI.

Majukumu ya kazi za kila siku za kitengo kidogo cha Usimamizi wa ardhi:-

  • Ukusanyaji wa kodi ya pango la ardhi.
  • Uhamasishaji na umilikishwaji wa viwanja na mashamba.
  • Utatuzi wa migogoro ya ardhi.
  • Uelimishaji wa jamii katika masuala mbalimbali yahusuyo usimamizi wa ardhi na umiliki wake.
  • Ukaguzi wa viwanja na mashamba yaliyopimwa na kumilikiwa kwa mujibu wa sheria.
  • Uandaaji wa vyeti vya ardhi ya vijiji.
  • Uangizwaji na uboreshaji wa takwimu ya ardhi katika mfumo wa kompyuta (integrated Land rent management system).
  • Na mengineyo yanayopangwa na mkuu wa idara/Mkurugenzi Mtendaji.

KITENGO KIDOGO CHA UPIMAJI NA RAMANI.

Majukumu ya kazi za kila siku za kitengo kidogo cha Upimaji na ramani:-

  • Kupima viwanja na mashamba.
  • Kuchora ramani za viwanja na mashamba.
  • Kuchora ramani za hati (DEED PLAN).
  • Kuonyesha mipaka ya vijiji na viwanja.
  • Kupeleka ramani za upimaji kuidhinishwa na Mkurugenzi wa upimaji na ramani.
  • Kutatua migogoro ya ardhi inayohusiana na masuala ya upimaji na ramani.
  • Kuandaa gharama zote zinazohusiana na miradi ya upimaji wa maeneo ya uuma pamoja na watu binafsi.
  • Kupokea maombi ya upimaji wa mashamba na viwanja.
  • Kuchora ramani za vijiji na maeneo ya utawala katika Wilaya.
  • Kutoa ushauri kwa masuala yanayohusu upimaji na ramani.
  • Kufanya kazi za nje ya ofisi (Field survey operation) chini ya usimamizi wa mpima aliyesajiliwa.

KITENGO KIDOGO CHA MISITU.

 

Majukumu ya kazi za kila siku za kitengo kidogo cha Misitu:-

  1. Kushughulikia shughuli zote za kitalu na kusimamia wahudumu wa kitalu ikiwemo kufanya usafi, kujaza viriba na umwagiliaji.
  • Kutembelea Wadau wa misitu kutoa Elimu ya Utunzaji wa Misitu, Uvunaji na Usafirishaji wa mazao ya Misitu.
  1. Kushughulikia shughuli zote za kitalu na kusimamia wahudumu wa kitalu ikiwemo kufanya usafi, kujaza viriba na umwagiliaji.
  2. Kutembelea Mashule ambayo tumeanzisha vitalu vya miche ya miti jumla ya shule nane .
  3. Kufanya Doria kwenye Misitu ya Hifadhi inayomilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, misitu hiyo ni Nyabasi n Bwiregi.
  4. Kutembelea wafanyabiashara wa Mazao ya Misitu kwa ajili ya kukagua vibali vya biashara ya mazao ya misitu.

 

KITENGO KIDOGO CHA WANYAMAPORI.

 

Majukumu ya kazi za kila siku za kitengo kidogo cha Wanyamapori:-

  1. Kushughulikia shughuli zote zinazo husiana na wanyama pori
  2. Kutembelea vijiji vyote vinavyo zunguka na hifadhi na kutoa elimu jinsi ya kupambana na wanyama waharibifu
  3. Kutembelea Mashule vijiji na kufanya tadhimini ya mashamba yaliyo haribiwa na tembo, nyati etc.
  4. Kufanya Doria kwenye maeneo yote yaliyopo pembezoni mwa hifadhi kwa lengo la kupunguza vitendo vya ujangili.
  5. Kufanya Doria kwenye maeneo yote yaliyopo pembezoni mwa hifadhi na yaliyopo chini ya halmashauri kwa lengo la kupunguza vitendo vya ujangili.

Matangazo ya Kawaida

  • MAELEZO YA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA KWA SHULE ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME December 13, 2020
  • KUITWA KWENYE USAHILI UANDIKISHAJI NA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA July 30, 2019
  • KUITWA KWENYE MAFUNZO August 02, 2019
  • TANGAZO KWA UMMA November 01, 2019
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA ENEO LA KUJENGA OFISI ZA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME KIJIJI CHA NYAMWAGA.

    February 17, 2021
  • Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kulipa deni la sh milioni 185 MSD.

    February 03, 2021
  • Mafunzo ya semina kwa waheshimiwa Madiwani kuwajengea uwezo wa kusimamia uwendeshaji wa halmashauri.

    January 19, 2021
  • MAAGIZO YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI ALIYOYATOA WAKATI WA ZIARA YAKE WILAYANI TARIME YATEKELEZWA KWA KISHINDO.

    May 21, 2020
  • Angalia Vyote

Video

MBUNGE WA TARIME VIJIJINI AWATUA MZIGO WA MICHANGO WANANCHI WAKE,AMWAGA SARUJI MIFUKO 660
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • strategic plan
  • Mfumo wa Kibali cha kusafiri nje ya nchi
  • Muongozo wa Mtumiaji Mfumo wa kibali cha kusafiri

Viungio Vinavyoshabiana

  • Government portal
  • TAMISEMI
  • HALMASHAURI WILAYA TARIME.BLOG
  • Taarifa za mshahara
  • Mfumo wa TANePS
  • Sajili mali iliyopotea

Idadi ya waliotembelea tovuti kidunia

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 GWF zimehifadhiwa