• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Mail za Ofisi |
    • Malalamiko |
TARIME DISTRICT COUNCIL
TARIME DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi na Awali
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Maendeleo ya Miundombinu Vijijini na Mjini
      • Maendeleo ya Jamii,
      • Mipango na Uratibu
    • Kitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Shughuli za Kilimo
    • Shughuli za Ufugaji
    • Shughuli za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha, Mipango & Utawala
      • Elimu, Afya & Maji
      • Mazingira, Ujenzi & Uchumi
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopangwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Taratibu Mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za Shughuli Mbalimbali
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

IDARA YA ARDHI YASISITIZWA KUTUMIA MFUMO WA UKUSANYAJI KODI

Tuma: March 12th, 2018

Naibu Waziri wa ardhi nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula ameiagiza halmashauri ya wilaya ya Tarime kuwafatilia wadaiwa sugu wa kodi za Ardhi zaidi ya Bilioni 3, na kwa wale watakaokaidi agizo hilo mali zao ziuzwe kulingana na thamani ya pesa wanayodaiwa.

Hayo aliyasema wakati wa Ziara yake Tarime ya kukagua mfumo wa ukusanyaji kodi za ardhi, na kuangalia hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Halmashauri katika ukusanyaji wa kodi ya ardhi ikizingatiwa kuna idadi kubwa ya wadaiwa sugu ndani ya Wilaya, pia hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Halmashauri katika kushughulikia migogoro ya mipaka.

Mabula aliwataja baadhi ya wadaiwa sugu wa kodi za ardhi wanaodaiwa tangu 1999 akiwemo Mzee Magarya Mwita ambaye anadaiwa zaidi ya shilingi milioni 80.

“Kanisa la Anglican milioni zaidi ya 478, Mara Cooparative milioni 205, MC Chambili milioni 58, Wilson Tanzania Limited milioni 28 ,Willison Kiguha milioni 19, Sylvesta Nyamuhanga milioni 17, Tarime English Medium milioni 4 na Tarime wood and Treatement milioni 6.’’

Aliongeza “hawa ni baadhi nimewataja kwa majina makusudi ili muwafahamu, Maafisa ardhi wafuatilieni watu hawa, serikali imewarahisishia kazi mnaingia kwenye mfumo na orodha yote mnaipata”.

Wakieleza changamoto mbalimbali zinazokabili Idara ya Ardhi, Kaimu Afisa Ardhi Halmashauri ya wilaya ya Tarime Rhoida Nyondo alisema migogoro mingi inashindwa kutatuliwa kutokana na wananchi kutokubaliana na ramani za Serikali na kutaka mipaka ya koo itambulike.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Tarime Moses Misiwa alimtaka Waziri huyo kuingilia kati mgogoro wa ardhi kijiji cha Gibaso na mwekezaji Isaack and Son anayedaiwa kuchukua eneo kinyume cha sheria ambapo Waziri aliagiza yafanyike marekebisho ya hati ya umiliki.

Waziri huyo aliwataka watumishi wa idara ya ardhi siku tatu katika wiki waende vijijini kutatua kero za wananchi, na kusisitiza suala la upimaji maeneo yote ya taasisi za umma ili kuepuka uvamizi.

,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,Mwisho,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Matangazo ya Kawaida

  • ORODHA YA VITAMBULISHO VYA WATUMISHI WA MAKAO MAKUU March 20, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA (DAFTARI LA WAPIGA KURA). April 19, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA February 25, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZIYA MKATABA KWA MADEREVA. May 30, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI

    February 20, 2025
  • TANZIA

    March 15, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MARA ATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME

    February 26, 2025
  • MHE. EVANCE MTAMBI AFANYA MKUTANO NA WANANCHI WA KATA YA MWEMA NA RWGICHERI JUU YA CHANGAMOTO YA ARDHI

    February 24, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Maadhimisho ya Nanenane, 2024
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • eMrejesho
  • Dirisha la Watumishi
  • Taarifa za Mishahara
  • NeST-Mfumo wa kielektroni wa manunuzi Tanzania
  • Mfumo wa Usajili Mali iliyopotea
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa wafanyabiashara wadogowadogo
  • Mfumo wa Kibali cha kusafiri nje ya nchi
  • STAFF ASSESSMENT

Viungio Vinavyoshabiana

  • Government portal
  • TAMISEMI
  • HALMASHAURI WILAYA TARIME.BLOG
  • Magazeti mbalimbali
  • Jarida la Tarimedc
  • MWALIMU WETU MITIHANI MBALIMBALI

Idadi ya waliotembelea tovuti kidunia

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 GWF zimehifadhiwa