• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Mail za Ofisi |
    • Malalamiko |
TARIME DISTRICT COUNCIL
TARIME DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi na Awali
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Maendeleo ya Miundombinu Vijijini na Mjini
      • Maendeleo ya Jamii,
      • Mipango na Uratibu
    • Kitengo
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Hesabu
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Kitengo cha Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Shughuli za Kilimo
    • Shughuli za Ufugaji
    • Shughuli za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha, Mipango & Utawala
      • Elimu, Afya & Maji
      • Mazingira, Ujenzi & Uchumi
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopangwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Miongozo
    • Fomu mbalimbali
    • Taarifa
    • Taratibu Mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video za Shughuli Mbalimbali
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

KIKAO KAZI CHA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA MAENDELEO

Tuma: October 20th, 2021

Mheshimiwa Col. Michael Mangwela Mntenjele Mkuu wa Wilaya ya Tarime katika kikao kazi kilichojumuisha Wakuu wa Idara, Waratibu elimu kata, walimu wakuu, wakuu wa shule na waganga wafawidhi wa vituo vya afya  kilichofanyika tarehe 20/10/2021 katika ukumbi wa shule ya sekondari JK Nyerere Nyamwaga kwa ajili ya kutoa maelekezo juu ya usimamizi wa miradi mipya ya maendeleo katika Halmashauri ya wilaya ya Tarime itakayotekelezwa kwa fedha za mapambano dhidi ya uviko 19 takribani shilingi bilioni 2.54 na tozo za miamala ya simu kiasi cha shilingi milioni 300.

Mkuu wa wilaya aliwaasa na kuwataka Watumishi katika ngazi zote kusimamia miradi hiyo kwa umakini, uadilifu, ubora na uaminifu na kwamba mfumo utakaotumika kutekeleza ni ule wa “force account”. Pia aliwataka watumishi wasimamie miradi kwa kufuata sheria na miongozo ya serikali bila kurubuniwa na mtu yeyote, na kwamba atakaekiuka utaratibu hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Aidha alikijulisha kikao kuwa tayari orodha ya vifaa hitajika na gharama za ufundi zimekwisha kutolewa kwa kila aina ya jengo na kusambazwa Tanzania nzima (schedule of materials). Hata hivyo alisema, suala la bei ya vifaa lazima kuzingatia bei ya soko na fedha zilizotolewa si kwa ajili ya kulipa posho, na kwamba kazi zote ziendane na muda uliopangwa huku ikizingatiwa thamani ya fedha (value for money).

Katika kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Ndugu Solomoni I. Shati alitoa utangulizi wa maelekezo ya namna  bora ya usimamizi wa miradi ya maendeleo kwa watumishi wa kada ya Elimu na Afya. Mkurugenzi pia alimshukuru Mhe Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutupatia fedha kiasi cha shilingi bilioni 2.84 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi na Halmashauri kwa ujumla.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji amemhakikishia Mkuu wa Wilaya kuwa fedha zote zilizotolewa zitasimamiwa kuhakikisha zinatumika ipasavyo, kwani tayari zimeshaundwa kamati za usimamizi kutoka ngazi ya kijiji hadi Mkoa na kwamba kama Wilaya tutatoa ushirikiano wa kiutendaji kwa kamati zote ili kufikia malengo pangwa.Akitaja kamati ya wilaya ya usimamizi miradi ya maendeleo inayoundwa na:-

Mhe Mkuu wa Wilaya……Mwenyekiti

 Mkurugenzi Mtendaji……Katibu

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya……Mjumbe

Afisa Usalama wa Wilaya (DSO)……Mjumbe

Afisa wa TAKUKURU Wilaya……Mjumbe

Mhandisi Ujenzi Wilaya……Mjumbe

Wakuu wa Idara na watumishi wa kada ya Elimu na Afya ambao ni maafisa elimu kata, wakuu wa shule, walimu wakuu na wasimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya, wakipokea maelekezo ya usimamizi bora wa miradi mipya ya maendeleo. 

Matangazo ya Kawaida

  • ORODHA YA VITAMBULISHO VYA WATUMISHI WA MAKAO MAKUU March 20, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA (DAFTARI LA WAPIGA KURA). April 19, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA February 25, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZIYA MKATABA KWA MADEREVA. May 30, 2024
  • Angalia Vyote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI

    February 20, 2025
  • TANZIA

    March 15, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MARA ATEMBELEA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME

    February 26, 2025
  • MHE. EVANCE MTAMBI AFANYA MKUTANO NA WANANCHI WA KATA YA MWEMA NA RWGICHERI JUU YA CHANGAMOTO YA ARDHI

    February 24, 2025
  • Angalia Vyote

Video

Maadhimisho ya Nanenane, 2024
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • eMrejesho
  • Dirisha la Watumishi
  • Taarifa za Mishahara
  • NeST-Mfumo wa kielektroni wa manunuzi Tanzania
  • Mfumo wa Usajili Mali iliyopotea
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mfumo wa wafanyabiashara wadogowadogo
  • Mfumo wa Kibali cha kusafiri nje ya nchi
  • STAFF ASSESSMENT

Viungio Vinavyoshabiana

  • Government portal
  • TAMISEMI
  • HALMASHAURI WILAYA TARIME.BLOG
  • Magazeti mbalimbali
  • Jarida la Tarimedc
  • MWALIMU WETU MITIHANI MBALIMBALI

Idadi ya waliotembelea tovuti kidunia

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 GWF zimehifadhiwa